Manispaa ya Ilala imemzuia mgombea
Urais wa UKAWA, Edward Lowassa kuzindua kampeni yake kwenye viwanja vya
Jangwani Jumamosi ya 29 Agosti, 2015.
Msemaji wa UKAWA ambaye pia ni Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, James Mbatia
amesema Manispaa ya Ilala imewagomea kufanya uzinduzi wa kampeni zao kwenye viwanja hivyovya Jangwani kwa madai kuwa
tayari kuna mtu mwingine ambaye ameshalipia uwanja huo.
Mbatia anasema pamoja na kufanya juhudi za kuomba kutajiwa aliyelipia uwanja huo ili wazungumze naye lakini halibado ilikuwa ngumu hawajaweza kutajiwa mtu huyo aliyelipia.
Mbatia anasema viongozi wengine wa UKAWA
wanashughulikia suala hilo ikiwa pamoja na kumtaka Mwenyekiti wa Tume
ya Uchaguzi, Damian Lubuva kuingilia kati.
0 comments :
Post a Comment