Taarifa zilizopo kwa sasa ni kuvamiwa kwa nyumba ya msanii wa Bongo
fleva Ali Kiba iliyopo maeneo ya Kunduchi ambayo anaishi na mdogo wake Abdu Kiba.
Abdu Kiba, amesema yeye alikuwa Masaki, Ali akampigia simu kwamba kuna watu kama 15 hivi wamevamia nyumbani kwao..
waliovamia waliruka ukuta saa tisa usiku, wakavunja mlango wa sebuleni,
wakakuta vijana wawili ambao wanaishi nao, wakawapiga na kuwalazimisha
wawaoneshe chumba ambacho Ali yupo.. wale vijana wakajibu kwamba Ali hayupo, wakaulizia chumba chake wakaoneshwa chumba cha Abdu Kiba.
Wameingia chumbani wakamkosa Ali Kiba, wameiba vitu vingi vya sebuleni na chumbani pia, pamoja na pesa milioni 2 na nusu zilizokuwa chumbani kwa Abdu.
Askari walifika na kukagua, wakaondoka na kuahidi kwamba wanafanya upelelezi.
Wakati tukio lote linaendelea Ali alikuwa ndani kwenye chumba kingine, hawakuomuona.
0 comments :
Post a Comment