Fid Q na Joh Makini ni rappers ambao wamekuwa wakichukuliwa kama hawaivi
chungu kimoja, na wakati mwingine wamekuwa wakishindanishwa na mashabiki wanaotaka
kujua nani mkali zaidi ya mwenzake.
Fareed “Fid Q” Kubanda ametoa mtazamo wake wa kile anachodhani kuwa sababu ya
mashabiki wa muziki wa Hip Hop kumshindanisha na rapper mwenzake Joh Makini kwenye
mitandao.
“Labda ni kwasababu (Joh) anaweza akawa ni msanii ambaye
anafanya vizuri kwahiyo wanakuwa wanamshindanisha na msanii mwenzake mwingine (Fid)
ambaye anafanya vizuri, lakini sidhani kama kuna kitu personal na siko katika position
kuamini mi nahitaji kushindanishwa na Joh.” Alisema Fid kupitia 255 ya XXL ya Clouds
Fm.
Fid amesema kuwa yeye ni msanii ambaye hawezi kushindanishwa na msanii mwingine
yeyote kutokana na kile anachokifanya kuwa tofauti na wanachofanya wasanii wengine wote,
na pale anaposhindanishwa huwa anaona kama amedharaulika.
“Nadhani wanaoshindanisha wajifunze kuwa wanafatilia watu wanaotaka
kuwashindanisha kwanza, mi nadhani niko tofauti kidogo na wanamuziki wengi sana ambao
wanafanya Hip Hop na hiyo haijalishi kama ngoma zangu zinapigwa sana redioni au
hazipigwi. Kibongobongo kiukweli mi sidhani naweza kushindanishwa na mtu na wala siwezi
kujisikia vizuri, na mara nyingi naposhindanishwa na mtu naona kama nimedharaulika hivi,
sio kwasabbu huyo mtu mwingine ni dhaifu No!, kwasababu mi nafanya kitu cha tofauti
sana…nazingatia zaidi uandishi, nafanya show mpaka kesho na ngoma kama dotcom,
dotcom ni ngoma ambayo nimeitoa 2003, 2004. Katika show zangu hizo hizo napigaga
Mwanza Mwanza ambayo imetoka 2005 ilikuwa nyimbo bora ya Hip Hop…saizi ni 2015
unaongelea miaka tisa iliyopita na zaidi, basi hebu tuangalie basi na hao wengine ambao
wanataka kunishindanisha nao wana vibao vyao vina miaka hiyo tisa ambavyo wanaweza
kufanya sasa hivi vingapi?”
Kuhusu kama amewahi kuwa na matatizo yoyote na Joh Makini:
“Sijawahi kuwa na matatizo na Joh Makini, nadhani matatizo yanayosikika kwa
watu.
Unajua fans wana vitu vyao, ukiingia sehemu mara utakutana na mtu kaweka picha sijui
Fid Q vs Joh Makini nani noma, nadhani vitu kama hivyo ndo waga vinatengeneza chokochoko nyingi
nyingi ambavyo mtu kama sio mtu wa kufikiria vyema unaweza kuchukulia personal.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments :
Post a Comment