Tuzo za kimataifa kwa wasanii wa Tanzania zinazidi kuongezeka siku hadi siku. Vanessa Mdee aka Vee Money atangazwa kuwania tuzo za African Entertainment Awards kwenye kipengele cha ‘Best International African Female Artist’. Hit maker huyo wa ‘No Body But Me’ ametoa taarifa hiyo kupitia akaunti yake ya Instagram kwa kuandika maneno haya:
“Namshukuru Mungu kwa nomination nyingine hii ya #AEA ya Canada. Ni Baraka kusema la ukweli Asanteni guys najua nguvu zenu pia zimechangia haya basi tupige kura. Link iko kwenye bio yangu Twitter @VanessaMdee #AwardSeason”
Tuzo hizo zitatolewa September 5, 2015 huko Mississauga, ambalo ni jiji la sita kwa ukubwa nchini Canada.
0 comments :
Post a Comment