Tamasha kubwa la kuadhimisha miaka kumi na sita ya msanii JUMA NATURE maarufu kama kiroboto pamoja na hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi jumamosi hii ya tarehe 30 mwezi mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala, kuanzia saa kumi na mbili jioni.
Tamasha kubwa la kuadhimisha miaka kumi na sita ya msanii JUMA NATURE maarufu kama kiroboto pamoja na hitimisho la sherehe za mwaka mmoja za 93.7 EFM linalofahamika kama KOMAA CONCERT
kwa mara ya kwanza litafanyika rasmi jumamosi hii ya tarehe 30 mwezi
mei katika ukumbi wa Dar Alive –Mbagala, kuanzia saa kumi na mbili
jioni.
Tamasha hili limeandaliwa na Juma nature
akishirikiana na EFM kwa lengo la kuwaburudisha Mashabiki wa juma
nature na wasikiliazaji wa 93.7 EFM ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru
mashabiki kwa ushirikiano wao kwa miaka kumi na sita ya muziki tangu
kuanza msanii huyo Juma Nature aingie kwenye game ya Muziki nchini
Tanzania.
Aidha, mashabiki watapata burudani
kutoka kwa kiroboto ambaye atatumia dakika 180 akiwa jukwaani
kuhakikisha anakonga nyoyo za mashabiki wake ambapo ataimba nyimbo zake
zote kali zilizofanya vizuri na kusindikizwa na wasanii kibao.
Miongoni mwa wasanii hao ni pamoja na Profesa Jay, Shetta, Snura, Makomando, Msagasumu na wengine wengi.
Tunatoa wito kwa mashabiki wote wa juma
nature , Efm Radio, wadau na wengine kujitokeza kwa wingi siku ya
tamasha hili ili kupata burudani hii ya kihistoria ambapo kiingilio
kitakuwa ni shilingi 7,000 tu.
Tunaamini Juma nature ni msanii mwenye
kipaji kikubwa na aliyewahamasisha wasanii kibao kuingia katika muziki
huu wa kizazi kipya hivyo anastahili kupewa heshima kubwa kwa mchango
wake mkubwa katika kukuza muziki wa kizazi kipya
Lakini kwa Efm huyu ni msanii wa Kwanza itaendelea kufanya hivyo kwa wasanii wengine kwakuwa kwetu sisi tunaamini
Muziki unaongea.
IMETOLEWA NA,DENIS SSEBO,
MENEJA MAWASILIANO NA MAMBO YA SHERIA WA EFM.
0 comments :
Post a Comment