Kweli mziki wa bongo fleva umekuwa chanzo kikubwa cha vijana kupata ajira zaidi pamoja kuweza kuendesha maisha yao bila kutegemea pamoja na kuliongezea taifa mapato. Dancer wa Diamond Platnumz aka Dangote ameonyesha kuwa mziki unalipa siyo kwa wasanii peke yao hata kwa dancers pia baada ya kununua ndinga mpya aina ya GASSO.
Diamond Platnumz
ni mmoja ya wasanii ambao wana mafaniko sana katika ukanda huu wa Afrika
ya Mashariki, Mafanikio ya Diamond yameweza kunufaisha pia Dancers
wake.
Diamond Platnumz kupitia mtandao wa Instagram ameandika “Huwa
nafarijika na kumshukuru sana Mwenyezi Mungu ninapoona vijana wenzangu
ninaofanya nao kazi licha ya kidogo tukipatacho ila wanakuwa na akili ya
kukitumia kimaendeleo… Mwenyezi Mungu akuongeze akili na maarifa ufanye
mengi mazuri zaidi ya hili @dumyutamu @dumyutamu @dumyutamu“.
0 comments :
Post a Comment