Manager wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho ameonyesha jeuri yake baada ya kumpiga marufuku daktari wa timu hiyo Eva Carneiro kuwa sehemu ya kikosi cha Chelsea kwenye mashindano yote wanayoshiriki miamba hiyo ya London.
Wawili hawa wameingia kwenye utata huu baada ya Mourinho kumshutumu Eva kwa kitendo cha kukimbia uwanjani kumtibu Eden Hazard akidhani ameumia vibaya wakati wa mchezo wao dhidi ya Swansea City.
Hii si mara ya kwanza kwa Mourinho kulumbana na madaktari wa timu yake na wakati mwingine hata timu pinzani kwani kwa nyakati tofauti akiwa kocha wa Chelsea , Inter Milan na Real Madrid wamewahi kuingia kwenye malumbano na matabibu .
0 comments :
Post a Comment