Msanii mkongwe wa mziki wa Hip Hop hapa Bongo, Joseph Haule a.k.a Professor Jay amechukua fomu ya kuwania Ubunge kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia jimbo la Mikumi mkoani Morogoro.
Hii imekuja baada ya kushinda kwa kishindo kwenye kura za maoni zilizokuwa zinafanyika ndani ya chama ili kumpata mgombea mmoja atakaye wakilisha Jimbo.
Haya ni maneno ambayo ameyaandika Prof Jay kwenye account yake ya Instagram..'Nimechukua fomu ya kugombea ubunge jimbo la MIKUMI kwa mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa Mr. Idd Mshili ambaye ndie msimamizi msaidizi wa Uchaguzi.. Eeh MWENYEZI MUNGU NISAIDIE’ – Professor Jay
-
Blogger Comment
-
Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments :
Post a Comment